Tue, 5 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kinara wa Magoli Ligi Kuu Tanzania Bara mpaka sasa, Kiungo wa Azam FC, Feisal Salum amesema kwamba;
“Sipendi kushindanishwa na mtu, naomba nifanye kazi yangu kwa kutumia kila nafasi nitakayoipata bila kumtazama nani ananifuata, lakini pia naheshimu uwezo wa Aziz Ki ambaye ni mchezaji mzuri.
Endapo atafunga mabao mengi kunizidi nitampongeza na mimi nikifunga mengi kumzidi nitashukuru na nitakuwa nimeonesha utofauti na misimu mingine kwa kufunga mabao mengi zaidi".
Mpaka sasa Feisal ana mabao 11, huku Aziz KI akiwa ameweka wavuni mabao 10.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live