Fri, 28 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
fahamu: Mchezaji wa kwanza wa Young Africans SC kuifunga KMC FC bao kwa mara ya kwanza kabisa tangu ilipopanda daraja na kuingia Ligi Kuu ni Feisal Salum 'Fei Toto'.
Fei aliifunga KMC Oktoba 25, mwaka 2018 ambapo alipiga mpira wa adhabu baada ya Heritier Ebenezer Makambo kufanyiwa madhambi na mchezaji wa KMC.
Bao lake la juzi, Oktoba 26, 2022 ni bao la tatu la Feisal dhidi ya Wakusanya Kodi hao wa Kinondoni KMC FC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live