Sat, 5 Aug 2023
Chanzo: Mwanaspoti
Kiungo wa Azam Fc ,Feisal Salum amesema ni bahati kuungana na Yanick Bangala katika klabu ya AzamFC.
Feisal amesema anaona ni jambo jema kwake kufanya kazi pamoja kama ambavyo walifanya pamoja wakiwa Yanga SC kwa sasa lengo ni kuipatia mataji timu yao mpya.
Bangala alijiunga na Yanga msimu wa 2021/22 na kumkuta Fei Toto aliyeingia Yanga tangu msimu wa 2018/19 lakini mwisho wa msimu uliomaliza 2022-2023 wachezaji hao waliondoka Yanga katika mazingira tofauti na kuuzwa Azam FC.
Je, unaiyona Azam ya Feitoto na Bangala ikibeba makombe mangapi msimu mpya?
Chanzo: Mwanaspoti