Familia ya nyota wa Liverpool Luis Diaz imeripotiwa kutekwa na watu wasiojulikana wakati wakiwa kwenye gari kuelekea nyumbani kwao m jini Barrancas, La Guajira Colombia.
Watu wenye silaha waliokuwa kwenye pikipiki waliivamica familia hiyo na kuwachukua kwenye gari lao na kuwapeleka kusikojulikana.
Hata hivyo Rais wa Colombia, qustavo Petro amethibitisha kwamba mama wa mshambuliaji huyo wa Colombia, Cilenis Marulanda ameokolewa huku maafisa wakiendelea na msako kumtafuta baba yake ambaye badlo hajapatikana.
Diaz (26) aliyejiunga. na Liverpool mnamo Januari z022 akitokea FC Porto ya Ureno bado hajazungumzia tukio hilo lakini Shirikisho la Soka Nchini Colombia katika taarifa yake limesikitishwa utekaji nyara huo na kuzitaka mamlaka husika kumuokoa baba wa ryota