Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Fahamu kuhusu kanuni ya michuano ya CAFCL

Maxi Yangaa (29).jpeg Fahamu kuhusu kanuni ya michuano ya CAFCL

Fri, 5 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Young Africans pamoja na kwamba inahitaji ushindi ili iweze kutinga hatua ya Nusu Fainali, inahitaji pia sare yoyote ya mabao ili kuweza kuiondosha Mamelodi Sundowns mashindanoni, kwani itabebwa na bao la ugenini, huku yenyewe ikiwa haijaruhusu bao lolote ikicheza nyumbani.

Kanuni za ligi hiyo zinasema hakutokuwa na muda wa nyongeza timu zitakapomaliza kwa sare yoyote ile, badala yake itaangaliwa aliyeshinda bao la ugenini, au mabao mengi ugenini ili kupata mshindi na kama timu zote zitakuwa zimetoka sare zinazofanana nyumbani na ugenini, basi moja kwa moja zitakwenda kupigiana mikwaju ya Penati baada ya dakika 90 za mchezo.

Kanuni hiyo pia inasema hata timu ikishinda idadi ya mabao kama yale ambayo mpinzani wake ameshinda katika mechi ya kwanza, basi moja kwa moja watakwenda kwenye mikwaju ya Penati na si kuongeza dakika.

Kwa maana hiyo, Young Africans ilitoka suluhu tena ya bila kufungana na wapinzani wao, na Simba ikashinda bao 1-0 Cairo, basi mikwaju ya Penati itahusika.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live