Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids amesema kuwa aliingia na mpango mzuri kwenye mchezo wa nusu fainali ya Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga ndiyo maana aliwashika pabaya vijana wa Miguel Gamondi.
Mchezo huo uliopigwa katika Dimba la Mkapa, Alhamisi Agosti 8, 2024, Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0 na kufanikiwa kutinga fainali ya michuano hiyo ambapo watakutana leo na Azam FC.
"Tunaujua ubora wa Aziz Ki na Pacome lakini tuliwanyamazisha kasoro moment moja tu ikaamua mechi"
“Nadhani tumeonesha utofauti kati ya timu iliyokaa miaka mitatu pamoja dhidi ya sisi ambao tumekaa wiki nne tu pamoja, tumeonesha hakuna utofauti kati ya hizi timu mbili, huoni utofauti wa miaka mitatu na wiki nne zetu, ” amesema Fadlu Davids.