Wed, 10 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Ligi Kuu ya NBC ya Singida Fountain Gate FC, imefungiwa kusajili mpaka itakapomlipa aliyekuwa mchezaji wao Shafik Batambuze.
Uamuzi huo umefanywa na FIFA baada ya mchezaji huyo kushinda kesi ya madai dhidi ya klabu hiyo.
Mchezaji huyo raia wa Uganda alifungua kesi FIFA akidai malipo ya ada ya usajili na malimbikizo ya mishahara.
Klabu hiyo ilitakiwa iwe imemlipa ndani ya siku 45 tangu uamuzi huo ulipotolelewa lakini haikutekeleza hukumu hiyo.
TFF nao wameifungia Singida kufanya uhamisho wa ndani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live