Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

FIFA waichunguza Senegal kwa kuvunja sheria Qatar

Senegal Gal FIFA waichunguza Senegal kwa kuvunja sheria Qatar

Wed, 30 Nov 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wapinzani wajao wa England kwenye Kombe la Dunia Senegal, wanachunguzwa na FIFA kwa kuvunja sheria nchini Qatar.

Wawakilishi wa Afrika watamenyana na England katika hatua ya 16 bora Jumapili baada ya kuifunga Ecuador mabao 2-1 katika mechi ya mwisho ya Kundi A.

Lakini Senegal wamejitupa kwenye maji moto kabla ya pambano lao dhidi ya kikosi cha Gareth Southgate kwa kutofuata kanuni za Kombe la Dunia.

Kabla ya mechi yao na Ecuador siku ya Jumanne, kocha wa Senegal Aliou Cisse alihudhuria mkutano wake na waandishi wa habari kabla ya mechi bila mchezaji wake mmoja.

Sheria za FIFA zinasema kwamba meneja lazima aambatane na mtu kutoka kwenye kikosi chake, katika vyumba vya mkutano na waandishi wa habari katika kituo kikuu cha habari huko Doha.

Cisse alionekana akiwa na mshambuliaji wa Monaco, Krepin Diatta kabla ya Senegal kufunga bao la kwanza dhidi ya Uholanzi.

Kalidou Koulibaly, aliyefunga bao la ushindi dhidi ya Ecuador dakika ya 70, kisha akashiriki pamoja naye kabla ya ushindi dhidi ya Qatar. Beti mechi zijazo za kombe la dunia na nyingine kupitia Meridianbet, beti na kitochi bila bando, kwenye machaguo spesho ya kombe la dunia yenye ODDS kubwa na bomba, na kama sio mpenzi wa mpira kuna michezo ya kasino mtandaoni napo unaweza kushinda jakipoti kubwa. Beti hapa.

Lakini Cisse alichagua kuzungumza na vyombo vya habari akiwa peke yake mapema wiki hii, huku FIFA ikisema kuwa hatua sasa itachukuliwa dhidi ya FA ya Senegal.

Taarifa ya iliyotoka mapema siku ya Jumatano ilisomeka: “Kamati ya Nidhamu ya FIFA imefungua kesi dhidi ya Shirikisho la Soka la Senegal kutokana na uwezekano wa ukiukaji wa kifungu cha 44 cha Kanuni za Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022, kifungu cha 2.7.2 cha Kanuni za Vyombo vya Habari na Masoko. na kifungu cha 8.5.3 cha Mwongozo wa Timu.

“Ukiukaji unaowezekana unahusiana na mkutano wa lazima wa waandishi wa habari ambao ulifanyika tarehe 28 Novemba kabla ya mechi ya Ecuador dhidi ya Senegal Kombe la Dunia la FIFA.”

Kuna uwezekano mkubwa kwamba Senegal itapewa faini pamoja na Ujerumani ikipata adhabu ya paundi 8,800 kwa kosa lile lile mapema kwenye michuano hiyo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live