Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

FIFA kuongeza idadi ya wachezaji Kombe la Dunia

Infatino Gianni Rais wa FIFA, Gianni Infantino

Fri, 24 Jun 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

FIFA imethibitisha kuwa itaruhusu timu kuchagua wachezaji 26 kwa ajili ya Michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Qatar.

Kila timu hapo awali iliruhusiwa kuwa na wachezaji 23, lakini FIFA imeongeza idadi ya vikosi vya Kombe la Dunia hadi kufikia wachezaji 26 mwaka huu, kutokana na janga la Covid-19.

FIFA pia ilisema hadi wachezaji 15 wa akiba wanaweza kutajwa kwenye mchezo, ikimaanisha kwamba hakuna mchezaji atakayekosa nafasi. "Nadhani kila mtu lazima awepo kwa michezo yote," alisema mnamo Aprili. Southgate aliongeza: "Ikiwa vikosi vitakuwa vikubwa basi inatakiwa kuwa hali ambayo kila mtu anaweza kubadilika siku ya mechi."

Tarehe ya mwisho kwa nchi zote 32, kuwasilisha vikosi vyao vya mwisho ni tarehe 20 Oktoba, siku 30 kabla ya mchezo wa kwanza kati ya Senegal na Uholanzi kwenye Uwanja wa Al Thumama.

FIFA pia ilisema si zaidi ya watu 26 hadi wachezaji 15 wa akiba na maafisa 11 wa timu, ambapo mmoja wao lazima awe daktari wa timu, wataruhusiwa kukaa kwenye benchi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live