Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

FIFA Yatoa maagizo kwa timu ya Taifa ya Urusi

Skysports Fifa Football 5570529 1536x864 FIFA Yatoa maagizo kwa timu ya Taifa Urusi

Mon, 28 Feb 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) limeitaka Urusi kucheza michezo yake katika Uwanja huru na bila mashabiki ikiwa ni kikwazo baada ya majeshi ya nchi hiyo kuivamia Ukraine na kuishambulia.

Hata hivyo, FIFA imesema timu za Urusi zitashiriki mashindano yote ya bodi hiyo ya soka duniani, ikiwemo Kombe la Dunia baadaye mwaka huu nchini Qatar.

Lakini FIFA imesema katika michezo ya Urusi hakutapeperushwa bendera ya nchi yao wala kuchezwa wimbo wa taifa lao.

FIFA imesema agizo hilo litaanza kwenye michezo ya mchujo wa kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Poland Machi ambao ulipangwa kuchezwa Jijini Moscow, Licha ya Poland kupanga kususia mchezo huo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live