Mon, 12 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
FIFA imeuonyesha mpira wake mpya ulioandaliwa kwa ajili ya nusu fainali na fainali za Kombe la Dunia 2022 zinazoendelea nchini Qatar.
Mpira huo umepewa jina la Kiarabu la "Al Hilm" likiwa na maana ya "Ndoto" (The Dream).
Timu ya Taifa ya Argentina ndio itakuwa ya kwanza kuutumia mpira huo katika mechi yao dhidi ya Croatia Jumanne usiku.
Mpira uliokuwa ukitumika hadi sasa katika kombe la dunia nchini Qatar ulijulikana kama" Al Rihla", ikiwa na maana ya "Safari" ( The Journey).
Chanzo: www.tanzaniaweb.live