Kutoka insta live ya Msemaji wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe, juzi akiwa na Rais wa Yanga, Eng. Hersi Said aliwapa Wananchi breaking news ya moto.
Eng. Hersi amesema kuwa katika msimu huu wa usajili dirisha kubwa, kuna mchezaji mmoja uyo fundi akisajiliwa, itatengenezwa bango kubwa lenye picha ya mchezaji huyo alafu litabandikwa opposite na jengo la timu moja hapa nchini.
Yani kwenye moja ya jengo la timu fulani, yanga itakodisha jengo linalo angaliana na jengo la timu hiyo alafu ilojengo liliokodiwa na yanga itabandikwa bango kubwa la mchezaji huyo, ili hiyo timu itakayo kuwa jirani apo iwe inamuona ona kwenye picha.
Na picha hiyo itaishi kwenye jengo Hilo Kwa muda wa miezi 6.
Unadhani atakua mchezaji gani huyo na hiyo picha itawekwa jirani na jengo la timu gani?