Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Everton kushushwa Daraja

Everon FC 10 Points Everton kushushwa Daraja

Fri, 17 Nov 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Everton itashushwa daraja baada ya kubaini kukiuka taratibu za matumizi ya fedha ambayo klabu hiyo imefanya na hii imekuja baada ya tume huru inayohusiana na mambo hayo masuala hayo.

Klabu ya Everton watapokwa alama 10 na kushushwa daraja moja kwa moja kutokana kukutwa na hatia hiyo kufanya udanganyifu katika matumizi na mapato klabuni hapo.

Kikawaida klabu yeyote nchini Uingereza inatakiwa ifanye matumizi kulingana na mapato ambayo yanaingia kwenye klabu hiyo, Endapo ikibainika klabu imefanya matumizi makubwa kuliko kiasi kinachoingia kwenye klabu ni wazi imevunja taratibu.

Klabu ya Everton baada ya uchunguzi wa tume huru inayofatilia masuala ya matumizi na faida nchini Uingereza wamebainika kua walifanya udanganyifu kwa kipindi cha nyuma kilichopita kupitia sajili zao.

Klabu hiyo inaelezwa imewasiiliana na mamlaka juu ya kukata rufaa kwajili ya kupingana na adhabu hiyo ambayo itawafanya kushuka daraja na kupokwa alama 10, Hii ikiwa na habari ya kusikitisha kwa mashabiki, viongozi, na wachezaji wa klabu hiyo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live