Fri, 27 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imesukumizwa nje ya michuano ya African Football League kufuatia kipigo cha jumla cha 3-1 dhidi ya vigogo wa Tunisia, Esperance de Tunis.
Mabao ya Esperance katika mchezo wa jana yamewekwa wavuni na Oussema Bouguerra aliefunga mabao mawili na Mohamed Tougai.
Mazembe ilishinda 1-0 katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa katika dimba la Benjamin Mkapa kabla ya kukubali kichapo cha 3-0 ugenini katika dimba la Olympique Hammadi Agrebi mjini Rades, Tunisia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live