Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Eriksen kurejea uwanjani

Https   S3 Images Christian Eriksen alipata madhara waati wa michuano ya Euro

Wed, 5 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Jina la Christian Eriksen bado halijapotea kwenye uso wa wanamichezo. Uwezo wake katika safu ya kiungo ushambuliaji, ni alama ya ubora wake uwanjani.

Eriksen alipata tatizo la moyo wakati akiitumikia timu ya Taifa ya Denmark kwenye mashindano ya Euro 2020. Toka amepata tatizo hilo ambalo liligusa hisia za watu wengi duniani, Christian anaendelea na matibu wakati huu ambao amewekea kifaa maalumu kwenye mfumo wake wa moyo.

Kwa kule nchini Italia ambapo alikuwa anaitumikia klabu ya Inter Milan, wachezaji wenye vifaa hivyo hawaruhusiwi kucheza kwenye Serie A. Sababu hii ilipelekea Inter na Christian kufikia makubaliano ya kusitisha mkataba baina yao.

Kwa sasa, Eriksen yupo nchini Denmark akifanya mazoezi na klabu ya Odense Boldklub ambayo aliwahi kuitumikia alipokuwa kijana mdogo.

Kwa mujibu wa wakala wa Christian, endapo mchezaji huyo atapata nafasi ya kurejea nchini Uingereza, itakuwa ni kama anarudi nyumbani. Ni nafasi ambayo ataihusudu kutokana na maisha aliyoyaishi nchini Uingereza alipokuwa na Spurs ambayo aliitumikia kwa miaka 7.

Tutegemee kumuona fundi huyu wa kutengeneza nafasi na kufunga magoli ndani na nje ya boksi ndani ya EPL kwa mara nyingine?

Chanzo: www.tanzaniaweb.live