Nyota wa timu ya taifa ya Argentina Enzo Fernandez amefanikiwa kuchukua tuzo ya mchezaji bora kijana wa michuano ya kombe la dunia 2022, ambapo nyota huyo mpaka hivi sasa ana miaka 21 tu na hii ikiwa ni michuano yake ya kwanza ya kombe la dunia kushiriki.
Mchezaji huyo anaekiputa kwenye klabu ya Benfica ya nchini Ureno ametangazwa kuwa mchezaji bora kijana michuano ya Kombe la Dunia 2022 iliyomalizika kwa timu ya Taifa ya Argentina kuibuka washindi na kunyakua kombe hilo mbele ya mabingwa watetezi Ufaransa.
Fernandez ameweza kuisaidia timu yake ya Taifa kubeba kombe hilo akiwa pia na mabao manne kwenye michuano hiyo.