Mkufunzi wa Newcastle United Eddie Howe ameiweka kando klabu hiyo kwenye mpango wa kumnunua mchezaji bora chipukizi wa kombe la dunia Enzo Fernandez anayelengwa na Liverpool.
Kiungo huyo wa kati wa Benfica mwenye umri wa miaka 21 kwa sasa yuko kwenye mbingu ya 9 baada ya kushinda Kombe la Dunia akiwa na Argentina nchini Qatar, lakini uchezaji wake katika kipindi chote cha michuano hiyo umemfanya afuatiliwe na vilabu kadhaa maarufu barani Ulaya, wakiwemo Liverpool wanaoonekana kuitaka kwa nguvu saini yake.
Matajiri wa Newcastle ni timu nyingine ya Ligi Kuu ya Uingereza ambayo imehusishwa na kutaka kumnunua nyota huyo aliekulia katika Academy ya River Plate baada ya mchezaji wa zamani Alan Shearer ‘kutania’ moja kwa moja kwenye TV baada ya fainali ya Qatar kwamba ataonekana mzuri katika rangi nyeusi na nyeupe kucheza dhidi ya Bournemouth katika Kombe la Carabao siku ya Jumanne.