Timu ya Taifa ya England "Three Lions" imezima ndoto za Timu ya Taifa ya Senegal jana Disemba 4 baada ya kuichapa mabao 3-0 hatua ya 16 bora Michuano ya Kombe la Dunia.
Senegal ndio timu kutoka bara la Afrika ambayo ilikuwa inapewa nafasi kubwa ya kufanya vyema katika michuano hiyo na pengine kuweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kufika nusu fainali ya michuano hiyo kutoka bara la Afrika.
Magoli ya England katika mchezo huo yamefunga na kiungo Jordan Henderson 38', Harry Kane 45+3 na Bukayo Saka kipindi cha pili dakika ya 57.
Kiungo Jude Belligham alionesha kiwango bora katika mchezo huo akitoa pasi ya bao kwa henderson lakini akihusika katika utengenezaji wa bao la pili la Harry Kane
Kuondolewa kwa Senegal kunafanya bara Afrika kubaki na mwakilishi mmoja tu ambae ni Morocco anaekabiliana na Hispania siku ya Jumanne.