Mon, 11 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Yanga SC, Injinia Hersi Said leo usiku atakuwa sehemu ya waalikwa watakaoshuhudia Mubashara Tuzo za Mchezaji Bora Afrika CAF.
Hersi ambaye pia ni Mwenyekiti wa vilabu vya soka Barani afrika (ACA) atakuwepo katika tuzo hizo zitakazofanyika nchini Morocco.
Hersi jana alishiriki mchezo wa kirafiki uliochezwa nchini humo na alikutana na magwiji mbalimbali wa soka la Afrika.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live