Wed, 15 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Yanga Eng. Hersi Said ametoa tafsiri ya nyota 3 zinazoonekana kwenye T-shirt za ubingwa walizovaa wachezaji, viongozi na baadhi ya mashabiki wa Yanga SC baada ya kutangazwa kuwa mabingwa wa Ligi kuu Tanzania bara 2023-24.
Hersi amesema kwenye hizo nyota 3 ni tafsiri sahihi ya makombe 30 ya Ligi Kuu, kila nyota inabeba makombe 10.
Yanga wametwaa ubingwa wa Ligi msimu huu baada ya kuibuka na ushindi wa Mabao 3-1 dhidi ya Mtibwa Sugara jana jioni na kufikisha alama 71 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote ile.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live