Fri, 24 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Yanga SC Mhandisi Hersi Said amepigiwa makofi Bungeni Jijini Dodoma na Wabunge waliokuwa katika Majadiliano ya Bajeti ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Mwaka 2024/25.
Hersi yuko na kikosi cha Yanga SC katika Bunge hilo walikopata mualiko maalum na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Damas Ndumbaro.
Rais huyo alipotambulishwa Bungeni hapo alisimama na kupigiwa makofi kwa sekunde 30 na kuibua shangwe ndani ya Bunge hilo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live