Mon, 29 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Yanga Eng. Hersi na Makamu wake Arafat Haji wamefanikiwa kumrejesha kazini Ally Kamwe kwenye nafasi yake ya Meneja Habari na Mawasiliano na Tayari amesaini Mkataba Mpya wa miaka miwili ndani ya Klabu hiyo.
Hii ni baada ya saa chache zilizopita, Ally Kamwe aliaga rasmi ndani ya kikosi hicho cha mitaa wa Twiga na Jangwani baada ya kuhudumu kwa miaka miwli.
Kamwe alieleza changamoto zake kwa viongozi zilizompelekea kuchukua uamuzi wa kujiuzulu mbele ya Uongozi na kwa maslahi ya pande zote mbili wamekubaliana kuzifanyia kazi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live