Tue, 28 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Klabu ya Young Africans, Eng. Hersi Said amewaambia Wananchi kwamba bado kiungo wao, Pacome Zouzoua tuna mdai pakubwa sana.
Eng. Hersi amesema kutokana na uwezo mkubwa alionao Pacome raia wa Ivory Coast, msimu huu ameuonyesha kidogo hivyo bado ana deni kubwa la kulipa.
“Huyu bado tunamdai sana, kama kuna mchezaji mwenye uwezo na hajatuonyesha uwezo wake kwa inavyotakiwa ni huyu, hivyo bado tunamdai.
“Huyu Pacome tunamdai, huyu akicheza kwa kiwango chake kile cha juu hakuna atakayemsogelea Afrika sio Tanzania pekee,” alisema Eng. Hersi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live