Baada ya wengi kuwa na mashaka na kiwango cha Yanga kwa siku za karibuni walianza kuweka mashaka katika mbinu za Mwalimu Miguel Gamondi.
Mchambuzi wa michezo kutoka Wasafi FM, Edo Kumwembe anasema;
“Kuna jambo la kujiuliza kuhusu ubora wa kocha aliyepita, Nasireddine Nabi na kocha wa sasa Miguel Gamondi. Ngumu kujua tofauti yao kwa namna Yanga inavyocheza. Kuna watu wamekuwa na wasiwasi na Gamondi baada ya hivi karibuni Yanga kusuasua katika ufungaji.Hata hivyo ukifuatilia namba unaweza kuona kuwa Gamondi anaweza kuwa bora kuliko Nabi mpaka sasa. Tunapaswa kusubiri na kuona mpaka mwishoni nani ataibuka mbabe.”