Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dyabala ashindwa kuvumilia maumivu

Gettyimages 841351906 1024x1024 Dyabala akiwa na Messi

Sat, 13 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Fowadi wa Juventus Paulo Dybala ametajwa kumwambia mchezaji mwenzake wa Argentina Angel Di Maria kwamba hangeweza ‘kuvumilia tena’ baada ya mchaka mchaka dhidi ya beki wa Uruguay Joaquin Piquerez.

Piquerez aliugonga mguu wa kushoto wa mshambuliaji huyo wa Juventus wakati wa Mechi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia kati ya Uruguay na Argentina, na Dybala akasalia chini kidogo kabla ya kuendelea.

Nyota huyu alijitahidi kusalia uwanjani kwa muda uliosalia wa kipindi cha kwanza, lakini kwa mujibu wa TyC Sport mchezaji huyo alikiri kwa winga wa Paris Saint-Germain Di Maria kwamba hangeweza kuendelea.

“Fideo, siwezi kuvumilia tena,” alimwambia mwenzake uwanjani, sentensi ambayo kamera zilimnasa akisema.

Kocha wa Argentina Lionel Scaloni aliamua kumtoa wakati wa mapumziko, akiwa na matumaini kuwa nyota huyo wa Juventus atapatikana kwenye mechi dhidi ya Brazil Jumanne.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live