Mchezaji wa Manchester City, Jérémy Baffour Doku amesema kuwa hajawahi kuona mchezaji Bora kwa Ligi ya Uingereza, Hispani na Italy kama Cristiano Ronaldo.
Doku amesema kuwa wanaomfananisha Ronaldo na Messi ni kumkosea heshima Mreno huyo kwani kwa sasa hana wa kumfananisha naye huku akidai kuwa Messi ni mchezaji aliyeshingwa Ligi ya Ufaransa.
"Kama mchezaji hajaonesha ubora wake EPL kwangu ni mchezaji wa kawaida, CR7 ni Legend hapa England, Hispania, Italy na Ureno kwanini umlinganishe na mchezaji aliyefeli Ligue 1?
“Kumlinganisha Ronaldo na Messi ni matusi kwa Ronaldo, yule ni mchezaji mkubwa hakuna wakufika ubora wake,“ amesema Jérémy Baffour Doku.