Kiungo Christian Zigar atakuwa sehemu ya wachezaji wa kikosi cha Dodoma Jiji msimu huu mara baada ya uongozi wa timu hiyo kumtambulisha rasmi leo.
Zigar hucheza namba sita na nane ni raia wa Ghana msimu uliopita aliitumikia Biashara United ambayo imeshuka daraja na msimu huu itacheza Championship pamoja na Mbeya Kwanza.
Huu unakuwa usajili wa pili kwa Dodoma Jiji ambapo jana ulimtambulisha mchezaji mwingine raia wa Ghana Collins Opare kutoka timu ya Biashara United.
Mtendaji Mkuu wa Dodoma Jiji,Fortunatus John amesema mchezaji huyo amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuwatumikia walima zabibu hao.
Miongoni mwa majina ambayo yanatajwa kusajiliwa na timu hiyo na wanaosubiri kutangazwa ni Jimmy Shoji kutoka Mbeya Kwanza, Amaan Kyata kutoka Coastal Union, Hassan Mwaterema kutoka Kagera Sugar, Randy Bangala na wengineo ambao majina yao wamefichwa.