Sat, 4 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wenyeji, KMC wamechapwa mabao 2-1 na Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Dodoma Jiji yamefungwa na Zidane Sereri dakika ya tatu na Emmanuel Martin dakika ya 22, wakati la KMC limefungwa na Rashid Chambo dakika ya 32.
Kwa ushindi huo, Dodoma Jiji FC inafikisha pointi 15 na kusogea nafasi ya nne ikiizidi wastani wa mabao KMC baada ya wote kucheza mechi tisa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: