Thu, 26 Oct 2023
Chanzo: Mwanaspoti
Bao pekee la Christian Zigah dakika ya 40 limeipa Dodoma Jiji FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Oktoba 25 Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
Bao pekee la Christian Zigah dakika ya 40 limeipa Dodoma Jiji FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Oktoba 25 Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Kwa ushindi huo, Dodoma Jiji FC wanafikisha pointi tisa na kusogea nafasi ya tano, wakati Kagera Sugar inabaki na pointi zake nane nafasi ya nane baada ya wote kucheza mechi saba.
Chanzo: Mwanaspoti