Mon, 12 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
TIMU ya Dodoma Jiji FC imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
Emanuel Mtumbuka alianza kuifungia Mashujaa FC dakika ya 30, kabla ya Hassan Mwaterema kuisawazishia Dodoma Jiji FC dakika ya 43.
Kwa matokeo hayo, Dodoma Jiji FC inafikisha pointi 19 nafasi ya saba, wakati Mashujaa inafikisha pointi 10 nafasi ya 15 baada y wote kucheza mechi 15.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: