Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro amelipongeza Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF kwa kuwa na usimamizi mzuri wa Utawala bora ambao umewawezesha TFF kufanikisha mafanikio yao husika.
Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro amelipongeza Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF kwa kuwa na usimamizi mzuri wa Utawala bora ambao umewawezesha TFF kufanikisha mafanikio yao husika. Salamu za Pongezi za Waziri Ndumbaro zimewasilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Taifa, Ally Mayai ambaye ameyasema hayo leo Jumamosi Desemba 16, 2023 kwenye Mkutano Mkuu wa TFF mkoani Iringa.