Sat, 14 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezaji wa zamani wa Manchester United Jesse Lingard anakaribia kusaini katika klabu ya Saudi Pro League Al Ettifaq.
Klabu hiyo inanolewa na nahodha wa zamani wa England na Liverpool Steven Gerrard. Gerrard anataka kumsajili Lingard lakini itabidi asubiri hadi mwezi Januari kutokana na sheria za kusajili wachezaji wa kigeni Nchini Saudi Arabia.
Wachezaji wa kigeni Saudi wanapaswa wasizidi 8 kwenye orodha wa wchezaji wanaocheza mechi na mpaka sasa Al Ettifaq ina wachezaji 10 wa kigeni.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live