Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Diego Simeone Ataja Mambo Matatu ya Kufanya Atletico

Diego Simeone Atle Kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone

Sat, 25 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Diego Simeone amedhamiria kubadilisha mambo katika klabu ya Atletico Madrid wakiwa wamejikuta wapo kwenye fomu mbaya msimu huu.

Atleti walitarajiwa kutetea vyema ubingwa wao wa La Liga wakiwa na kikosi cha timu chenye ubora wa hali ya juu.

Lakini wanaelekea katika mapumziko ya Krismasi chini ya pointi 17 nyuma ya vinara wa ligi Real Madrid kufuatia kupoteza mechi nne mfululizo.

Los Rojiblancos wamepoteza mbele ya Mallorca, Atletico Madrid, Real Madrid na Granada hivi karibuni.

Huku kukiwa na nafasi ndogo ya kushinda Ligi ya Mabingwa, msimu wa Atleti unaweza kumalizika kwa upande wa kuwania mataji msimu huu, huku Copa del Rey pekee ikionekana kuwa kwenye unafuu zaidi kwao kwa wakati huu.

Lakini wakati presha inazidi kupanda, bosi wa Atleti Simeone amewaambia wachezaji wake mambo matatu ambayo wanapaswa kufanya ili kubadilisha mambo wakati wakielekea kwenye mapumziko ya Krismasi.

Baada ya kushindwa kwa Granada, Diego Simeone alisema ni wakati wa wachezaji wake: “Kuburudisha akili, kustarehe na kufanya kazi.”

Ukirejea kwenye misingi ya Atletico Madrid, na Simeone anajua vyema utaalamu wa vijana wake.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live