Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Diarra ni mwamba sanaa huyu jamaa

Diarra WA0004 Diarra ni mwamba sanaa huyu jamaa

Mon, 3 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Djigui Diarra ni Golikipa wa viwango vya juu sana, kabla ya penati kupigwa rudia mechi utaona aliwafuata Wachezaji wote wakiwa kwenye mstari na kuwaambia “Tumieni sana akili” alisisitiza kama mara mbili kuwa mikwaju inataka akili na utulivu, alirudia sana kwakuwa huwa wanampa sana kazi na anawajua vizuri.

Rejea tena video hata wakati Stephen Aziz Ki anaenda kupiga penati, ni kama Wachezaji walikuwa wamesimama tu, akasimama yeye na kuwaita kwa nguvu kuwa wanaanza wao kupiga penati ndipo Aziz Ki akaenda.

Rejea mechi ukipata muda kama sikosei penati ya tatu aligundua kuwa Kipa wa Azam ana mind game za hatari sana kwa wapigaji wake, akawa anasimama mbele kama anapiga yeye mpaka Mchezaji wake akisogea ndipo anatoka.

Mwisho rejea mechi ukipenda hii ya Azam ama ya Champions League dhidi ya Mamelodi Sundowns! Nadhani ndio Kipa pekee ambaye hatoki kwenye mstari kabla ya movement ya mpira, nadhani ni mafundisho makubwa aliyopata, hajawa nyanda kwa bahati mbaya, hata Kipa wa Azam nae alikuwa vizuri kwenye hilo kutotoka kwenye mstari kama wengine wengi.

Wengi hamkumzingatia kabisa, ila amefanya kazi kubwa sana kuituliza timu yake, amefanya kazi kubwa mno Diarra.

DIARRA WHAT A GOALIE.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live