Mchambuzi wa soka George Ambangile, amesema Diarra ni bora kuliko kipa wa Simba SC, Ayoub Lakred pindi wanapokuwa na mpira mguuni.
Amesema, Diarra ni daraja la juu kulinganisha na Aayoub katika kipengele wanapokuwa na mpira japo pia Ayoub kuna vitu anamzidi Diarra hususan katika mipira ya krosi kutokana na kuwa mrefu zaidi.
Takwimu za mchezo wa Simba na Yanga Kimataifa katika michezo yao iliyopita;
Diarra kagusa mpira mara 32, Akipiga pasi 26, 21 zikiwa pasi sahihi, Huku Ayoub kagusa mpira mara 46, Kapiga pasi 30, 19 zikiwa pasi sahihi, Kwa takwimu hizi ni wazi kuwa Diarra ni bora akiwa na mpira mguuni.