Tue, 21 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Golikipa wa Klabu ya Yanga, Djigui Diarra ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2023 iliyotolewa na kampuni ya kimataifa ya Magic Vibe Awards.
Diarra ametwaa tuzo hiyo akiwashinda Kibu Denis anayekipiga Tanzania, Fredinand Omanyala wa Kenya, Okot Benis wa Kenya na Jacob Kiplimo wa Uganda.
Tuzo hiyo ilitolewa usiku wa Novemba 19, 2023 katika Ukumbi wa Mlimani City.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live