Golikipa namba moja wa Yanga SC, Djigui Diarra na kiungo wao mshambuliaji Aziz Ki, hawatakuwa sehemu ya mchezo leo watakapokuwa kibaruani dhidi ya Dodoma Jiji FC.
Yanga waliotoka kuangusha alama mbili mchezo uliopita baada ya kutoka sare dhidi ya Kagera Sugar, watakuwa kwenye uwanja wa Azam Complex leo Februari 5, 2024 kuwakabili Dodoma.
Akiuzungumzia mchezo huo, Afisa Habari wa Yanga SC, Ali Kamwe amesema watawakosa nyota hao ambao bado hawajarejea nchini kutoka kwenye majukumu ya timu zao za Taifa katika michuano ya Afcon.
"Tumewapa siku mbili ambazo tunaamini watakuwa wamesharejea nchini na wataungana na timu," alisema Kamwe.