Juventus imeanza vyema michuano ya Euopa hatua ya 16 bora kwa kushinda bao 1-0 dhidi ya Freiburg inayoshiriki Ligi Kuu nchini Ujerumani Bundesliga huku ikiwa haina huduma ya Paul Pogba kutokana na utovu wa nidhamu klabuni hapo.
Pogba mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United, alichelewa kuijiunga na wenzake ambapo kocha wa Juve Max Allgeri aliamua kuachana naye kwenye mkondo wa kwanza uliochezwa Turin.
Bao pekee kwenye mechi hiyo limefungwa na mshindi wa Kombe la Dunia Qatar 2022, Angel di Maria, mchezo ujao utapigwa Alhamis ijayo Ujerumani.
Mechi nyingine, kocha Jose Mourinho ameiongoza AS Roma kuifunga bao 2-0 Real Sociedad.