Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dejan Kulusevski awapambanisha Spurs na Arsenal

Dejan Kulusevski 1536x1024 Dejan Kulusevski

Mon, 29 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Arsenal na Tottenham Hotspur wanaripotiwa kugombania saini ya mshambuliaji wa Juventus Dejan Kulusevski katika dirisha dogo la usajili la majira ya kiangazi.

Mchezaji huyo mwenye miaka 21 amecheza mechi 17 na Juventus, kwenye kampeni za 2021-22 lakini ameanza mara mbili pekee kwenye mechi za Serie A, mechi 15 za ugenini msimu huu akitokea benchi.

Hivi majuzi kumekuwa na taarifa kwamba Juventus iko tayari kumuuza mchezaji huyo wa kimataifa wa Uswidi ili kuongeza bajeti yao, huku ofa ya Euro milioni 35 (Pauni milioni 29.4) ikitajwa kuwa mezani.

Kwa mujibu wa Calciomercato, Arsenal na Tottenham wote wana nia ya kumleta mshambuliaji huyo kwenye Premier League na wanaweza kupambania saini yake mwaka ujao.

Kulusevski, ambaye ana uwezo wa kucheza katika nafasi mbalimbali za mbele, ameona nyavu mara nane na kusajili pasi nane za mabao katika mechi 64 alizoichezea Juventus kwenye mashindano yote.

Vilabu vingi vya Ulaya vinaaminika kutaka kumsajili Msweden huyo, lakini ripoti ya hivi majuzi ilidai kwamba kuhamia Ligi ya Premia ndiyo kuna uwezekano mkubwa zaidi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live