Wed, 6 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mara baada ya Jana kufanikiwa kuipa Arsenal alama tatu dhidi ya Luton Town kwa bao lake la ushindi dakika za jioni.
Kiungo wa Arsenal Decline Rice anasema akifanikiwa kufunga bao katika mechi basi hutumia muda mwingi kulitazama bao hilo.
Rice anasema hali hiyo inakuja kwa sababu yeye huwa hafungi magoli mara kwa mara anapokuwa Uwanjani.
Akizungumza mara baada ya Mchezo jana Rice anasema;
"Nikifunga goli huwa narudia rudia kuangalia sana, kwasababu huwa sifungi mara nyingi, hili goli naenda kuliangalia usiku mzima".
Chanzo: www.tanzaniaweb.live