Ukweli na uwazi ... Respect KDB . ( Sio wachezaji wengine wanapenda kutuona watoto eti hawafuati hela Saudi Arabia )
Kevin De Bruyne alipoulizwa kuhusu kucheza Saudi Arabia " Saudi ? Kwa umri wangu lazima ufungue mlango wa kila kitu . Tunaongelea kuhusu hela nyingi sana katika hatua ya mwisho wa maisha yangu ya soka , lazima ufikirie kuhusu hilo "
" Kama nikicheza huko kwa miaka miwili nitavuna kiasi kikubwa sana cha fedha , kabla ya hapo ilinibidi nicheze kwa miaka 15 na hata hivyo inawezekana nisifikie hizo fedha pia za miaka miwili "
"Nimebakiza mwaka mmoja ndani ya Man City kwahiyo utakuwa muda wa kufikiria na kuamua kuhusu mustakabali wangu "