Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

De Bruyne aingia katika vitabu vya kumbukumbu Man City

KDB DD Kiungo wa Man City, Kevin de Bruyne

Sun, 7 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mara baada ya jana kufunga mabao mawili kati ya manne waliyoshinda dhidi ya Crystal Palace, kiungo mshambuliaji wa klabu ya Man City na timu ya Taifa ya Ubelgiji Kelvin De Bruyne rasmi sasa ameingia kwenye orodha ya wachezaji waliofikisha mabao 100 kwenye klabu hiyo.

De Bruyne amefikia rekodi hiyo baada ya mechi 372 akiwa na uzi wa City huku akifikisha asisti 167 baada ya jana hiyo hiyo pia kupika bao safi kwa Erling Halland.

Kwenye mchezo huo City ambao City waliwafunga Palace mabao 4-2, magoli mengine ya City yamefungwa na Erling Halland na Rico Lewis.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live