Mon, 23 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Daniel Daga ni miongoni mwa wachezaji ambao wameweka historia ya kuwa mchezaji wa kwanza mwenye umri mdogo kucheza ndani ya michuano mipya ya African Football League (AFL) tangu kuanzishwa kwake.
Daga raia wa Nigeria ana umri wa miaka 16 anakipiga katika kikosi cha Enyimba Fc ya nchini Nigeria anacheza nafasi ya kiungo wa kati ndani ya timu hiyo.
Ameandika historia hiyo kwenye mchezo wa Enyimba Fc dhidi ya Wydad Casablanca ambao umepigwa katika dimba la Godswill Akpabio huko nchini Nigeria.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live