Wed, 20 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mahakama ya juu katika Jiji la Barcelona nchini Hispania imeamuru kuwa mchezaji wa zamani wa klabu ya FC Barcelona Dani Alves aachiliwe huru kutoka gerezani kwa dhamana mara baada ya wawakilishi wake kulipa kiasi Cha € Milioni Moja
Ufafanuzi ni kwamba ,Alves Bado ataendelea kuwa chini ya uangalizi maalumu wa kiulinzi kwa amri ya mahakama na anatakiwa kuwasili mahakamani kila wiki mara Moja mpaka pale hukumu yake ya miaka 4 na nusu itakapomalizika rasmi.
Alves alihukumiwa miaka minne na nusu jela kwa kosa la kumnyanyasa mwanamke mmoja kingono
Chanzo: www.tanzaniaweb.live