Tue, 10 May 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ikiwa wamefululiza Sare tatu mfululizo wakitoa sare tasa, tayari Mashabiki wa Timu ya Yanga wameanza kukata tamaa licha ya kuongoza msimamo wa Ligi kwa tofauti ya alama 11.
Yanga wamecheza michezo mitatu ya hivi karibuni pasipo kuibuka na ushindi wala kupata bao lolote.
Walitoa sare na Simba April 30, kisha wakasuluhu na Ruvu Shooting na jana mei 9 wamelazimishwa sare na Tanzania Prisons.
Msikilize Msemaji wa Yanga akizungumzia mipango ya timu kwa sasa kuelekea mchezo wao ujao hali kadhalika kile kinachozungumzwa na wapenzi wa Yanga.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live