Mabosi wa Simba wamemrejesha kikosini, Bernard Morrison, lakini wakimpa dakika 180 za mechi mbili zilizopo mbele yao ili kuona kama anapaswa kuendelea kubaki klabuni, licha ya kufahamu kila kitu juu ya kutakiwa na watani wao, Yanga.
Mabosi wa Simba wamemrejesha kikosini, Bernard Morrison, lakini wakimpa dakika 180 za mechi mbili zilizopo mbele yao ili kuona kama anapaswa kuendelea kubaki klabuni, licha ya kufahamu kila kitu juu ya kutakiwa na watani wao, Yanga. Awali, alipewa mechi tatu, lakini juzi usiku aliingizwa kipindi cha pili katika mchezo wa Kombe la ASFC dhidi ya Ruvu Shooting na aliisaidia timu hiyo kupata mabao mawili wakati Wekundu wakiwasasambua maafande hao kwa mabao 7-0.