Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dabi ya Sudan kupigwa Dar es Salaam

DYSGCXGC Dabi ya Sudan kupigwa Dar es Salaam

Tue, 25 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Chama cha Mpira wa Miguu nchini Sudan (SFA) kimetuma maombi kwenda Shirikisho la soka Tanzania (TFF) juu ya kuutumia uwanja wa Azam Complex, Chamazi kwa mashindano ya Sudan Super League inayotarajiwa kuanza kurindima kuanzia Juni 25 mpaka Juni 30, 2024.

Taarifa ya TFF imebainisha kuwa mashindano hayo yenye lengo la ujumbe wa kurudisha amani nchini Sudan yatashirikisha timu za Al-Hilal, Al-Merrikh na Al-Wadi Nyala.

Michezo hiyo ya Super League itachezwa kuanzia saa 12 jioni, Ratiba ipo hivi;

- Juni 25, 2024: Al-Hilal SC v Al-Wadi Nyala - Juni 27, 2024: Al-Wadi Nyala v Al-Merrikh - Juni 30, 2024: Al-Merrikh SC v Al-Hilal

Picha juu ni wachezaji zamani wa klabu hizo ambao wamewahi kupita Simba SC, Paschal Wawa aliyevaa jezi ya Al Merrikh na Sharaf Eldin Shiboub aliyevaa jezi ya Al Hilal.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live