Tue, 12 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
CAF wametangaza droo ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa ambapo Simba SC, wamepangwa na Al Ahly na kwa mujibu wa kanuni, Simba ataanzia nyumbani na kumalizia ugenini.
Faida ya Simba kuchezwa na Al Ahly, wanaifahamu vizuri kwani ametoka kucheza nao kwenye kombe la African Footbal, Simba alipata sare ya 2-2 nyumbani na ugenini akatoka 1-1 hivyo Al Ahly kuvuka kwa faida ya goli la ugenini.
Kama hiyo haitoshi, Simba kwa siku za karibuni, amekuwa akipata matokeo kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa.
Mechi ya kwanza ya nyumbani itapigwa kati ya 29-31, Marchi na za kurudiana baadaye Apili.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live