Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DONDOO ZA SOKA: Arsenal waendelea kusuka bomu la mauaji Ulaya

Mabeki Arsenal DONDOO ZA SOKA: Arsenal waendelea kusuka bomu la mauaji Ulaya

Tue, 5 Dec 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Arsenal wako karibu kufikia makubaliano wachezaji wao wawili wa safu ya ulinzi Takehiro Tomiyasu na Benjamin White juu ya kusaini mikata mipya kuendelea kusalia klabuni hapo.

kiungo Jorginho anatarajiwa kuondoka klabuni hapo mwishoni mwa msimu huu

Manchester City wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumsajili chipukizi wa Argentina Claudio Echeverri, ambaye tayari amepewa jina la 'Lionel Messi ajaye' baada ya kung'ara kwenye Kombe la Dunia la Vijana wa U-17.

Nyota huyo wa River Plate amezivutia klabu za Real Madrid, Barcelona, Paris Saint-Germain, Juventus, AC Milan na Inter Milan.

Juventus wanaweza kuwapa Jadon Sancho na Donny van de Beek njia ya kuondoka Manchester United msimu huu wa baridi. Wawili hao kwa muda mrefu wamekosa nafasi chini ya Erik ten Hag na wanaweza kupatikana kwa pauni milioni 26 tu mwezi ujao.

Juventus pia wanavutiwa na Kalvin Phillips kwa ajili ya kuimarisha safu yao ya kiungo.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza ameichezea Manchester City mechi nane pekee msimu huu huku akianza kwenye mechi moja ya Kombe la Carabao na amekuwa akihusishwa sana na kuondoka Etihad Januari.

Rais wa Atletico Madrid Enrique Cerezo amedai Joao Felix atarejea katika klabu hiyo, isipokuwa kama Barcelona wako tayari kufanya mkataba wake wa mkopo kuwa wa kudumu.

Mreno huyo alifunga bao la ushindi wakati Wacatalunya hao walipoichapa Atletico Jumapili usiku.

Kiungo wa kati wa Tottenham Pierre Emile-Hojbjerg pia yuko kwenye rada za Juventus, lakini shida ya majeraha ya Spurs inamaanisha Ange Postecoglou anaweza kusita kuondoka Mdenmark huyo.

Manchester United wamehusishwa kutaka kumnunua mshambuliaji wa Bayern Munich Thomas Muller. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 ameanza mechi nne pekee kati ya 12 za Bundesliga msimu huu na ametakiwa na nyota wa Ujerumani Lothar Matthaus kutafuta soka la kawaida nje ya Allianz Arena.

Manchester United inaweza kuwauza kiungo wa kati wa Uingereza Jadon Sancho, 23, na kiungo wa kati wa Uholanzi Donny van de Beek, 26, kwa Juventus kwa £26m pekee.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live