Sun, 23 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Yanga wanaikaribisha Simba SC muda mchache ujao katika Uwanja wa Benjamin Mkapa katika mchezo unaovuta hisia za wengi Ligi kuu ya NBC.
Timu zote zinavutana kileleni zikiwa na alama 13 huku Simba wakiwa juu kwa faida ya magoli mengi ya kufunga.
Yanga wamekuwa na rekodi nzuri katika michezo ya hivi karibuni wanapokutana na Simba kwani wamefanikiwa kuibuka na ushindi.
Tazama vikosi vinavyoanza mchezo wa leo kwa timu zote mbili.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live